Gurudumu La Uchumi

Informações:

Sinopse

Fahamu masuala kadha wa kadha kuhusu uchumi kama vile, namna ya kupambana na umaskini, mfumuko wa bei, kushamiri kwa matumizi ya dola na athari za kuyumba kwa uchumi wa dunia kwa nchi za Afrika. Mada hizi zinafanyiwa utafiti wa kina na zinazungumzwa kwa lugha rahisi inayoeleweka ili kukufanya uelewe na usichoke kusikiliza .

Episódios

  • MABADILIKO YA TABIA NCHI KWA UCHUMI

    10/08/2023 Duração: 10min

    Athari za mabadiliko ya tabia nchi kuanzia mafuriko na ukame zimesababisha mamilioni ya raia kupoteza makazi yao, wengi wakitumbukia katika hali ya umasikini na hata kufa njaa, baadhi wakikosa huduma muhimlu ya afya, elimu huku tofauti kati ya walionacho na wasionacho ikiendelea kuongezeka, uchumi wa mataifa ukidorora. Kwa mujibu wau moja wa Mataifa mpaka kufikia mwaka 2030 watu wanaokadiriwa kufikia milioni 700 huenda wakawa wakuhamahama kutokana na ukame peke yake.Kuchukua hatua stahiki kukabili mabadiliko ya tabia nchi na athari zake ni jambo lisilohitaji mjadala wa muda mrefu ili kunusuru maisha ya raia pamoja na kufikia malengo endelevu ya umoja wa Mataifa.Haya yanajiri wakati huu joto likiendelea kuongezeka, nchi zikitumia fedha nyingi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi badala ya kuwa zingeelekezwa katika kutatua changamoto za maendeleo na kiuchumi hasa kwenye nchi masikini.Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaangazia ni namna gani nchi zinazoendelea zinaweza kukabiliana na athari z

  • Je Afrika inawezaje kutumia raslimali watu kwa maendeleo ya uchumi?

    02/08/2023 Duração: 10min

    Takwimu zinaonyesha kuwa rasilimali watu katika nchi za kusini mwa jangwa la Sahara, ilikuwa ndogo mno ikilinganishwa na mataifa mengine ya dunia, ambapo Uviko 19 na vita vya Urusi nchini Ukraine vilichangia.  Wiki hii Emmanuel Makundi anaangazia wito wa wakuu wa nchi za ukanda ili kuangalia namna bora zaidi ya kutumia nguvu kazi iliyoko barani Afrika kwa maendeleo.

  • DRC: Kushuka kwa thamani ya fedha na changamoto la wakimbizi wa ndani

    26/07/2023 Duração: 09min

    Wimbi la wakimbizi wa ndani pamoja nakushuka kwa thamani ya pesa za kongo dhidi ya dola za Marekani  kumesababisha kupanda kwa gharama za maisha katika miji kadhaa nchini jamuhuri yakidemokrasia ya Kongo. Makal aya Gurudumu la uchumi juma hili inaangazia kwa kina hali hii na mtayarishaji Emmanuel Makundi, ameshirikiana na mwandishi wa Goma Benjamini Kasembe pamoja na kuzungumza na mtaalamu wa uchumi kutoka Bukavu Bengeya Machozi.

  • Ujuzi kwa vijana na teknolojia

    12/07/2023 Duração: 10min

    Makala ya Gurudumu la uchumi juma hili, inaangazia siku ya "ujuzi kwa vijana duniani' inayoadhimishwa kila tarehe 15 ya mwezi Julai kila mwaka, lengo ni kuwawezesha walimu, wakufunzi na vijana kutumia ujuzi wao kwa maendeleo.Leo mtayarishaji amezungumza na Tukupala Mwalyolo, msichana anayeunda ndege zisizo na rubani 'drone', pamoja na Emmanuel Cosmas Msoka, kijana mbunifu wote wakitumia teknolojia kutafuta suluhu na wako Tanzania.

Página 2 de 2